Yesu Wangu Niokoe
| Yesu Wangu Niokoe | |
|---|---|
| Performed by | St. Maurus Kurasini | 
| Album | Hubirini Kwa Kuimba | 
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) | 
| Composer | A. K. C. Singombe | 
| Views | 10,587 | 
Yesu Wangu Niokoe Lyrics
- Yesu wangu niokoe,
 { Ulimwegu nilimo ni wa mateso
 Nishike mkono wangu Bwana niokoe
 Ulikuja duniani kwa wadhambi,
 Nitakase kwa damuyo Bwana nitakate
 Bwana nakukimbilia } *2
- Nionyeshe uso wako uso mkunjufu, nisamehe dhambi,
 Nakusihi Mwokozi, Bwana unisikie
- Nimefanana na mwana mwana mpotevu, dhiki na karaha
 Vimenisonga sana Bwana unisikie
- Wewe ndiwe ngome yangu ngao yangu tumaini langu
 Ninakutegemea Bwana unisikie
- Roho yangu mwili wangu vyote ni vyako ndivyo ulivyoumba
 Viimarishe Bwana, Bwana unisikie
- Mungu Baba Mungu mwamba Mungu mkombozi
 Mungu wa mapaji, Utatu Mtakatifu usifiwe milele
 
  
         
                            