Tutawapeni Mapesa
| Tutawapeni Mapesa | |
|---|---|
| Alt Title | Haya Enyi Makamanda | 
| Performed by | St. Charles Lwanga Yombo Dovya Dsm | 
| Album | Kafufuka Mwokozi | 
| Category | Pasaka (Easter) | 
| Composer | A. S. Haule | 
| Views | 9,613 | 
Tutawapeni Mapesa Lyrics
- Haya enyi makamanda, leteni mchango wenu *2
 Nguvu ya hoja itawa-ale,
 Hawa walinzi wameleta habari kuwa kweli amefufuka, amefufuka *2
 Sikieni mimi natoa hoja ya nguvu, hoja yangu kweli ya nguvu
 Jambo hili likisikika, likisikika katika Uyahudi
 Na Samaria itakuwaje aibu hiyo elezeni *2
- Hivyo ninyi walinzi, seme-ni
 Wanafunzi wake wamemwiba Bwana wao *2
 Sisi tulipokuwa tumelala *2
- { (Tutawapeni mapesa) tutawapeni mapesa,
 Tutawajaza mapesa, mapesa mtajazwa } *2
 Na msiogope kwa ajili ya hilo * 2
 { Wakuu wa nchi wakisikia tutaongea nao
 Wakuu wa nchi hao tutasema nao } *2
 a. Siku ile ya kufufuka Bwana, maaskari walitetemeka
 Wakaenda kwa upesi kumwona jemedari mkuu kumpasha habari
- b. Jemedari akafadhaika akawaita watu pamoja kwa shauri;
 Wakafanya shauri juu ya jambo hili lipate sura, sura mpya.
- c. Dunia yetu siku hizi yafananaje na haya mambo yaliyotokea;
 Ukweli unapindishwa ili lile la uongo liwe kweli
Also recorded by St. Cecilia Arusha
  
 
 
 
  
         
                            