Ee Bwana Nifundishe Kupenda
   
    
     
         
          
            Ee Bwana Nifundishe Kupenda Lyrics
 
             
            
- Ee Bwana nifundishe kupenda, ee Bwana nifundishe kutumikia
 Ee Bwana nifundishe (kuwajua wenzangu ee) Ee Bwana nifundishe kutumikia
- Nifanye juhudi kuwajua watu, kusudi nizifahamu shida zao
 Nisiwape kazi kubwa kutafuta njia ya kunieleza shida zao
 Nisiwe mwenye haraka kuwachoka, niliowasaidia mara nyingi
 Nijue kusaidia ni safari, iliyo na milima mingi na miiba
- Nijue kuwatetea wadhaifu, wasipoteze thamani nikiona
 Maana hawakuchagua hali yao. Wamekuwa hivyo kusudi utukuzwe
 Nijibidiishe daima kutafuta, kuwasiliana na jamaa zetu
 Kwa kuwa mahusiano ni gharama, hayawezi kuwepo bila jitihada
- Maana nikishajua kupenda, na nikazingatia kutumikia
 Kilicho nileta hapa duniani, kitakuwa kimetia niondoke