Kimulimuli
| Kimulimuli | |
|---|---|
| Performed by | St. Joseph the Worker Ngokolo Shinyanga | 
| Album | Njooni Tumsifu Mungu | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | F. E. Nyanza | 
| Views | 3,694 | 
Kimulimuli Lyrics
- Kimulimuli chamulika pande zote za dunia
 Ngurumo zake zasikika, zasikika kote
 ona matetemeko ya ardhi, hata na vita
 pia na njaa nayo magonjwa yasipona
 Tuyakumbuke yale yaliyotabiriwa na manabii
 ya kuwa siku za mwisho yatatokea haya
 Tujiweke tayari atakapokuja Bwana wa mavuno
 Mbingu na nchi zitapita
 Neno la Mungu litadumu
 Tujiweke tayari atakapokuja Bwana wa mavuno
 Tujiweke tayari
 {Tujitakase, tujitakase, tujiweke tayari
 Tujitahidi, tubadili mwenendo wa maisha
 Kwa kuwa hatujui siku wala saa }* 2
- Tumuombe sana Mungu arudishe huruma yake
 Tuweze kushinda haya yote
 
  
         
                            