Sauti Inavuma

Sauti Inavuma
Performed bySt. Kizito Makuburi
AlbumYuko Galilaya
CategoryPasaka (Easter)
ComposerBernard Mukasa
Views11,800

Sauti Inavuma Lyrics

  1. Sauti inavuma (kulia), sauti inavuma (kushoto)
    Sauti inavuma pande zote zinatikisika ulo
    Dunia inanesa (kabisa), mbingu zinafurahi (lazima)
    Watumwa wako huru, wanaimba na kumshukuru Mungu
    Hii ni siku yetu, ya kubadilika na kutakata
    Kuvua utu wa kale, na kuvaa, kuvaa utu mpya leo
    Kwani mwalimu wetu, walimning`iniza na kumuua
    Kaachana na kaburi ni mzima kama alivyokuwa mwanzo
    Tunaimba aleluya, eeh eh aleluya,
    Tunaimba aleluya, tunamshukuru aliye juu
    Ngoma tunamchezea, tunamchezea,
    Vigelegele vya nguvu vinaambatana na makofi
    Tunapiga makofi makofi, makofi tu.

  2. Ya kibinadamu kayaishi kama, kama vile tulivyo sisi (kabisa)
    Na halafu akabadilika akavaa mwili wa utukufu
  3. Lengo lake atuelimishe hivi, hivi kabisa tulivyo sisi (kabisa)
    Tujitahidi kubadilika na kuvaa hali ya utukufu
  4. Tukubali maumivu yote tena tujikane bila kusaza (fahali)
    Makusudi tuzisalimishe hizi nafsi zetu kwa Mungu wetu