Acheni Ninyi Acheni Kabisa
| Acheni Ninyi Acheni Kabisa | |
|---|---|
| Alt Title | Wateteni Wanyonge na Yatima | 
| Performed by | St. Veronicah Kariakoo | 
| Album | Walinizunguka Kama Nyuki | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | F. Mtegeta | 
| Views | 4,125 | 
Acheni Ninyi Acheni Kabisa Lyrics
ACHENI NINYI
- Acheni ninyi, acheni kabisa, acheni kuwapendelea waovu
 Wateteeni wanyonge na yatima, wapeni haki masikini na fukara
 Waokoeni wanyonge na maskini katika makucha ya wadhalimu
- Acheni kutoa hukumu, hukumu isiyo ya haki kwa wanyonge
 {Kwa kuwa (kwa kuwa) wanyonge na maskini ni wa Mungu
 Msiwakandamize wanyonge kwa kuwatetea waovu } * 2
- Lakini ninyi hamjui, aliyewapa mamlaka ni nani
 Ni yeye (ni yeye) anaye uchukia uovu
 Anayeuchukia uovu na kuwapenda maskini
- Maisha ya dunia ni mafupi sana ndugu kumbukeni
 Na ninyi (na ninyi) mtakufa kama wakuu wengine
 Kama walivyokufa na kuyaacha madaraka na mali
 
  
         
                            