Ni Wewe Tu
| Ni Wewe Tu | |
|---|---|
| Alt Title | Kanuni Moja na Lugha Moja | 
| Performed by | St. Veronicah Kariakoo | 
| Album | Walinizunguka Kama Nyuki | 
| Category | Harusi | 
| Composer | Bernard Mukasa | 
| Views | 9,744 | 
Ni Wewe Tu Lyrics
- Kanuni moja na lugha moja kwako we
 Siku zote nitakupenda kweli ee
 Ya ulimwengu hayanibadilishi we
 Siku zote nitakupenda kweli ee (haya)Katika raha, (ni wewe) katika shida, tena ni wewe tu * 2
 Ni wewe tu, ni wewe tu (tena ) ni wewe tena ni wewe tu * 2
- Tumefinyangwa kwa tope moja sisi ee
 Ni pumzi moja imetutengeneza ee
- Ingawa ulimwengu mtamu sana ee
 Sitaujali kwani wewe ni zaidi
- Mapungufu yako nitayachukulia
 Na msamaha sitakawia kukupa
- Nitakupenda kama nilivyoagizwa
 Kama Kristu alivyolipenda kanisa
- Maisha yetu yakamtukuze Baba
 Yamuinue Mwana yampambe Roho
Recorded by 
* St. Veronicah Kariakoo 
* Mt. Yuda Thadei Mbeya
* Kapotive Singers Bukoba
  
 
 
 
  
         
                            