Kimeeleweka
| Kimeeleweka | |
|---|---|
| Alt Title | Kilichomfanya Baba Amtoe Mwanawe | 
| Performed by | St. Kizito Makuburi | 
| Album | Yuko Galilaya | 
| Category | Pasaka (Easter) | 
| Composer | Bernard Mukasa | 
| Views | 10,648 | 
Kimeeleweka Lyrics
- Kilichomfanya Baba amtoe mwanawe wa pekee
 Kilichomfanya mwana akubali kufa kifo cha aibu
 Leo kimefafanuliwa, leo kimeeleweka
 Leo kimefafanuliwa, kimeeleweka, kimeeleweka!
- Alimuona mwanadamu, anaanguka kuzimu
 Akaja kumuinua, akakibugia kifo
 Akashuka nacho, kuzimu kisha, akakiacha huko
- Alijua udanganyifu wa Ibilisi mzushi
 Akaja kuuharibu na kufunua ukweli
 Kuzigaragaza, hila za mwovu, na kumuaibisha
- Alimpenda mwanadamu, akampenda upeo
 Kajifanananisha naye bali hakutenda dhambi
 Akamuinua kiumbe huyu kampandisha hadhi
 // h i t i m i s h o //
 Amevishinda vita vya imani, mshindi
 Amevaa utukufu na enzi, Mwokozi
 Aeh atangaza mlango wa mbingu, u wazi
 Aeh na urithi wa utawala
 Kafufuka kama alivyosema yesu,
 Amefufuka, ameyashinda mauti
 Kafufuka (kafufuka) kama alivyosema Yesu,
 Amefufuka (kafufuka) ameyashinda mauti
 Kaivunja milango yote ya kuzimu,
 Ameivunja, ameyashinda mauti, kafufuka . . .
 Kaonyesha ya kwamba inawezekana,
 Ameonyesha ameyashinda mauti, kafufuka . . .
 Kwa hiyo, tuimbe aleluya ni shangwe kuu,
 Kwa hiyo, tuimbe aleluya kwani Bwana ameyashinda mauti
 Kwa hiyo, tuimbe aleluya ni shangwe kuu,
 Kwa hiyo, tuimbe aleluya kwani Bwana ameyashinda mauti
 Ameyashinda mauti, ameyashinda mauti,
 ame ame ame ame ameyashinda mauti
 
  
         
                            