Kimeeleweka

Kimeeleweka
Alt TitleKilichomfanya Baba Amtoe Mwanawe
Performed bySt. Kizito Makuburi
AlbumYuko Galilaya
CategoryPasaka (Easter)
ComposerBernard Mukasa
Views9,160

Kimeeleweka Lyrics

  1. Kilichomfanya Baba amtoe mwanawe wa pekee
    Kilichomfanya mwana akubali kufa kifo cha aibu
    Leo kimefafanuliwa, leo kimeeleweka
    Leo kimefafanuliwa, kimeeleweka, kimeeleweka!

  2. Alimuona mwanadamu, anaanguka kuzimu
    Akaja kumuinua, akakibugia kifo
    Akashuka nacho, kuzimu kisha, akakiacha huko
  3. Alijua udanganyifu wa Ibilisi mzushi
    Akaja kuuharibu na kufunua ukweli
    Kuzigaragaza, hila za mwovu, na kumuaibisha
  4. Alimpenda mwanadamu, akampenda upeo
    Kajifanananisha naye bali hakutenda dhambi
    Akamuinua kiumbe huyu kampandisha hadhi

    // h i t i m i s h o //
    Amevishinda vita vya imani, mshindi
    Amevaa utukufu na enzi, Mwokozi
    Aeh atangaza mlango wa mbingu, u wazi
    Aeh na urithi wa utawala

    Kafufuka kama alivyosema yesu,
    Amefufuka, ameyashinda mauti
    Kafufuka (kafufuka) kama alivyosema Yesu,
    Amefufuka (kafufuka) ameyashinda mauti

    Kaivunja milango yote ya kuzimu,
    Ameivunja, ameyashinda mauti, kafufuka . . .

    Kaonyesha ya kwamba inawezekana,
    Ameonyesha ameyashinda mauti, kafufuka . . .

    Kwa hiyo, tuimbe aleluya ni shangwe kuu,
    Kwa hiyo, tuimbe aleluya kwani Bwana ameyashinda mauti
    Kwa hiyo, tuimbe aleluya ni shangwe kuu,
    Kwa hiyo, tuimbe aleluya kwani Bwana ameyashinda mauti

    Ameyashinda mauti, ameyashinda mauti,
    ame ame ame ame ameyashinda mauti