Amka Ewe Usinziaye
| Amka Ewe Usinziaye | |
|---|---|
| Performed by | - | 
| Album | Kila Kunapokucha | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | Victor Aloyce Murishiwa | 
| Views | 4,363 | 
Amka Ewe Usinziaye Lyrics
- Amka ewe usinziaye, amka ewe usinziaye
 Amka, amka, fungua macho, amka
 Pesa ni kitu cha kushangaza
 Imezitega nyoyo za watu tazama,
 Tazama uaminifu hakuna
 Imejenga matabaka kwa maskini na matajiri, pesa
 Imekuwa ni kitanzi, inafilisha hata sheria, pesa
 Inagombanisha ndugu kwa ndugu pesa (tena)
 Imekuwa ndiyo mzizi wa tamaa
 Lakini ajabu ni kwamba,
 Pesa kamwe pesa kamwe,
 haitanunua mbingu ee Mungu
 kama matajiri wangemiliki hewa,
 maskini wangekuwa wapi
 Kama matajiri wangemiliki mbingu,
 maskini wangekosa haki
- Pesa ni rafiki kwenye shida zako
 lakini pesa ni adui kwenye raha zako
- Pesa yabadili msimamo wako
 Tazama pesa ni mbolea hustawisha dhambi
- Pesa ni mtego kwa imani yako
 Na tena pesa ni kioo kwa tabia yako
Recorded also by St. Claire Gatimu Kawangware, Nairobi
  
 
 
 
  
         
                            