Amka Ewe Usinziaye

Amka Ewe Usinziaye
Performed by-
AlbumKila Kunapokucha
CategoryTafakari
ComposerVictor Aloyce Murishiwa
Views3,733

Amka Ewe Usinziaye Lyrics

  1. Amka ewe usinziaye, amka ewe usinziaye
    Amka, amka, fungua macho, amka
    Pesa ni kitu cha kushangaza
    Imezitega nyoyo za watu tazama,
    Tazama uaminifu hakuna
    Imejenga matabaka kwa maskini na matajiri, pesa
    Imekuwa ni kitanzi, inafilisha hata sheria, pesa
    Inagombanisha ndugu kwa ndugu pesa (tena)
    Imekuwa ndiyo mzizi wa tamaa
    Lakini ajabu ni kwamba,
    Pesa kamwe pesa kamwe,
    haitanunua mbingu ee Mungu
    kama matajiri wangemiliki hewa,
    maskini wangekuwa wapi
    Kama matajiri wangemiliki mbingu,
    maskini wangekosa haki

  2. Pesa ni rafiki kwenye shida zako
    lakini pesa ni adui kwenye raha zako
  3. Pesa yabadili msimamo wako
    Tazama pesa ni mbolea hustawisha dhambi
  4. Pesa ni mtego kwa imani yako
    Na tena pesa ni kioo kwa tabia yako
Recorded also by St. Claire Gatimu Kawangware, Nairobi