Angalia Jinsi Mkulima

Angalia Jinsi Mkulima
Performed by-
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
ComposerPerfect Marandu
Views4,309

Angalia Jinsi Mkulima Lyrics

  1. {Angalia jinsi mkulima anavyofurahi-ya,
    Kuyachuna matunda (yale) yaliyoiva vizuri
    Katika bustani yake }* 2
    Na pia kuyatupa yale mabovu mbali
    Na kuyaacha yaliyo mabichi ili yapate kuiva vizuri
    ili aweze kuyachuma tena

  2. Vivyo hivyo Mungu hufurahia kuwaita kwake wale walio safi
    na kuwapa nafasi ya kutubu wale wenye dhambi
  3. Ni wajibu kwangu mimi na wewe,kutubu kwani hakuna ajuaye siku
    Wala saa ambayo Mungu Baba atamwita kwake
  4. Ewe ndugu yangu unafikiria nini kuingia katika jubilei
    Ya miaka elfu mbili ukiwa na mzigo wa dhambi
  5. Yafaa nini mtu kupata raha zote za dunia ambazo ni zam muda
    Na kutupwa katika moto ule wa milele yote
  6. Mimi na wewe tutumie nafasi hii tuliyopewa tutubu dhambi zetu
    Mtu asijeijutia siku atakayoitwa
Recorded also by St. Gabriel Biticha Kisii