Ninakushukuru Bwana
   
    
     
        | Ninakushukuru Bwana | 
|---|
| Alt Title | J. Mugangos | 
| Performed by | - | 
| Album | Haya Tazameni (Vol 21) | 
| Category | Thanksgiving / Shukrani | 
| Composer | J. Mugangos | 
| Views | 9,811 | 
Ninakushukuru Bwana Lyrics
 
             
            
- Ninakushukuru Bwana, ninakushukuru Bwana
 Kwa mema unayonijalia ninakushukuru
 Ninakushukuru Bwana
 mimi ninakushukuru Bwana mimi ninakushukuru Bwana
 Ninakushukuru Bwana
 mimi ninakushukuru Bwana mimi ninakushukuru Bwana
- Nina kila sababu ya kukushukuru Bwana
 (Tena) Tena inanipasa nitoe shukrani zangu,
 Kwako wewe Muumba wangu muumba wangu, ewe Mungu wangu
- {Ninatazama jinsi nilivyo mimi,
 ni wewe Bwana uliyeniumba mimi (Bwana)
 Ukanipa uzima, ukanipa uzima, pia na akili } * 2
- Na tazama na pia vitu vyote nilivyo navyo
 Nimevipata kutoka kwako Bwana Mungu wangu
 Kwa nini nisishukuru, kwa nini?
 Kwa nini nisikushukuru Bwana
 Kwa nini nisikushukuru Bwana
 Kwa nini nisikushukuru Bwana Muumba wangu
 (Yanipasa) Yanipasa nikushukuru
- { Ninakushukuru kwa moyo wangu wote
 Ninakushukuru Mungu wangu
 Ninakushukuru Mungu wangu
 Ninakushukuru Mungu wangu kwa moyo wangu wote } * 2
- Ninakusihi ewe Bwana Mungu wangu
 uzipokee shukrani zangu
 Ingawaje shukrani zangu hazilingani na wema wako kwangu, ee Mungu wangu
- Ninafahamu Bwana unanipenda, ingawaje
 Waujua udhaifu wangu na mawazo yangu yote ya kila siku
 Na maneno na matendo yangu yote
- Ninajiuliza nikushukuru jinsi gani Mungu wangu
 Nitakuimbia wimbo wa sifa
 Wimbo ule ulio bora wimbo wa shukrani, wa shukrani
 Niyatangaze matendo yako makuu
 Na sifa zako na wema wako wakati wote
 Na pia mahali pote
- Nitalitangaza Neno lako kwa watu wote, wakuheshimu wakufuate wewe
 Ninakuomba uniimarishe pia unilinde, ili nikufuate wewe daima na daima
 nami nitakushukuru siku zote za maisha yangu nisadie Bwana
- Ninakushukuru Bwana, ninakushukuru Bwana
 Kwa mema unayonijalia ninakushukuru
 Ninakushukuru Bwana, ninakushukuru Bwana
 Kwa mema unayonijalia ninakushukuru
- Ninatoa asante kwako Bwana Mungu wangu
 Asante, asante, asante,
 Ninatoa asante kwako Bwana Mungu wangu
 Asante, asante, asante,
- a-asante (asante), a-asante (asante) , a-asante (asante asante),
 asante asante asante (asante)
- a-asante (asante), a-asante (asante) , a-asante (asante asante),
 asante Mungu Baba asante