Mbinguni ni Furaha
   
    
     
        | Mbinguni ni Furaha | 
|---|
| Performed by | - | 
| Album | Uwe Nami Bwana | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | JohnBosco Hosea | 
| Views | 7,348 | 
Mbinguni ni Furaha Lyrics
 
             
            
- Nimeahidiwa utukufu mbinguni – Kwake Mungu Baba
 Nikamilishapo kazi yake Bwana – Aliyeniumba
 Nitatunukiwa tuzo za kifalme – nikiwa mshindi
 {t/b} Mbinguni ni furaha
 Tutaimba, na kucheza
 Tutaruka kwa furaha tukimwona Mungu,
 Tuendapo paradiso aliyotuandalia sisi wateule x2
- Nyimbo za ushindi mimi nitaimba – Nikimwona Mungu
 Sauti za mbinguni mimi nitapewa – naye Mungu wangu
 Nikiwa na kwaya tamu za malaika – wote wa mbinguni
 Tutaimba hosanna
- Makao ya kifahari mimi nitapewa – nilioandaliwa
 Yaliyo na urembo usio na mifano – ya dhamani kubwa
 Mandhari ya dhahabu na pia almasi – yanayometemeta
 Mbinguni kwapendeza.
- Nitashangilia nikiwa barazani – pamoja na Mungu
 Na watakatifu wake Mungu Baba – walionitangulia
 Karamu ya wateule tutaandaliwa – kufutwa machozi,
 Kwa shangwe na nderemo.
- Makao ya kifahari kweli ni mazuri – tena matulivu,
 Yasiyo na njaa shida wala kifo – furaha kila siku,
 Kazi ni kumsifu na kutukuza Mungu – milele amina
 Huko ndiko nyumbani.