Ee Mungu Nitakutafuta Mapema

Ee Mungu Nitakutafuta Mapema
Performed bySt. Monica Lower Kabete Campus UoN
AlbumUwe Nami Bwana
CategoryZaburi
ComposerJohnBosco Hosea
Views8,157

Ee Mungu Nitakutafuta Mapema Lyrics

  1. [ t ] Ee Mungu, mungu wangu ee Bwana
    [ w ] Nitakutafuta mapema, nafsi yakuonea kiu x2
    [ t ] Maana
    [ w ] Maneno yako ni Roho na uzima
    Wewe unayo maneno ya uzima wa milee x2
  2. [ s ] Ee Mungu, Mungu wangu, nitakutafuta mapema,
    Nafsi yakuonea kiu, mwili wakuonea shauku,
    Kwenye nchi kavu yenye uchovu,
    Nchi kavu isiyo na maji.
  3. [ t ] Ndipo nilikutazama, katika patakatifu,
    Nizione nguvu zako, na utukufu wako,
    Maana fadhili zako, ni njema kuliko uhai,
    Nafsi yangu itakusifu.
  4. [ a ] Ndipo nitakubariki, wakati mimi naishi,
    Nikiinua mikono yangu, nitaliomba jina lako,
    Kwa utajiri wa karamu, nafsi yangu imeridhika,
    Kwa midomo ya kinywa changu, nitakusifu wewe.
  5. [ b ] Wewe ni msaada wangu,
    Katika uvuli wa mbawa zako, hupiga kelele kwa furaha.
    Nafsi yangu hushikamana, haraka kwako Bwana,
    Kwa midomo ya kinywa cha-a-ngu, nitaku-usifu wewe.