Mimi ni Mkate wa Uzima

Mimi ni Mkate wa Uzima
Performed by-
CategoryEkaristia (Eucharist)
Composer(traditional)
Views6,682

Mimi ni Mkate wa Uzima Lyrics

  1. Mimi ni mkate wa uzima, ajaye kwangu hataona njaa.
    Mtu hawezi kunijia kamwe, asipovutwa na Baba yangu.

    Nitamfufua kweli, nitamfufua kweli
    Nitamfufua kweli, siku ya mwisho.

  2. Mkate huu ni mwili wangu, kwa uzima wa ulimwengu.
    Aulaye mkate huo, kweli ataishi milele yote.
  3. Mimi ni ufufuko, Mimi ni uzima,
    Yeye aniaminiye ajapokufa, atakua hai.
  4. Mimi ni njia, mimi ni mlango,
    Aingiaye kwa mimi, ataokoka na kushibishwa.
  5. Ee Bwana, twaamini, wewe ndiwe yule
    Mtakatifu wa Mungu, ulituletea kweli uzima.