Bwana Anachunga

Bwana Anachunga
Performed by-
CategoryZaburi
Composer(traditional)
Views4,922

Bwana Anachunga Lyrics

  1. Bwana anachunga uzima wangu,
    Na malisho yake raha tele
    Malisho mwake yale mabichi,
    Kamwe mimi sitapungukiwa.

    Bwana ndiye kweli mchungaji mwema
    Sitahitaji kitu chochote
    Penye majani yale mabichi, ndipo Bwana atanilisha.
    Sitahitaji, kitu chochote kitu chochote sitahitaji
    Penye majani yale mabichi yale mabichi penye majani.

  2. Penye maji mazuri matulivu,
    Ndipo anaponiburudisha
    Ananiongoza pasipo shaka
    Njia nzuri, adili na nyofu.
  3. Mabondeni mwa uvuli wa mauti
    Ninapopita sitaogopa
    Kwa maana Bwana yupo na mimi
    Gongo na fimbo vyako faraja.
  4. Meza waniandalia vitamu,
    Nitashiba mbele ya watesi
    Kichwa changu mafuta umepaka
    Kikombe changu chajaa mema
  5. Wema na fadhili zote za Bwana
    Zimenijia mpaka milele
    Ninaomba kwake mchungaji wangu
    Nikae kwake hata milele.