Bwana ni Mchunga

Bwana ni Mchunga
Performed by-
CategoryZaburi
Views14,463

Bwana ni Mchunga Lyrics

  1. Bwana ni mchunga, sitahitaji.
    Majani mabichi, malisho yangu.
    Ananinywesha maji matulivu
    Atanirudisha nikipotea
  2. Nipitapo bondeni mwa mauti,
    U mlinzi wangu, sitaogopa.
    Fimbo lako latosha kunilinda.
    Ukinifariji sina hasara.
  3. Kati ya mateso meza waandaa
    Na kikombe changu kinafurika
    Umenipaka kichwani mafuta.
    Nitaulizaje zaidi kwako.
  4. Wema na fadhili vinifuate
    Siku zangu zote, hata milele.
    Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana.
    Katika ufalme wa pendo lake.