Shangilia Harusi
   
    
     
        | Shangilia Harusi | 
|---|
| Performed by | - | 
| Category | Harusi | 
| Views | 4,427 | 
Shangilia Harusi Lyrics
 
             
            
- Yelele lele, yelele lele, leo tunayo furaha tele tele
 Twasherehekea arusi ya wenzetu
 Wamejitolea kwa moyo wao wote
 Twasherehekea yote wametimiza
 Arusi leo shangilia aa, shangilieni maarusi hawa
 Arusi leo furahia aa, furahieni maarusi hawa
- Twaombea baraka zake Bwana
 Munapoanza maisha haya mapya
 Shetani asiwatenganishe kamwe
 Mubaki ndani ya Bwana Mungu wetu
- Ewe mwanaume umpende mke wako
 Kwani hiyo ndiyo amri ya Mungu wetu
 Nawe mwanamke umpende mume wakao
 Ndipo ndoa yenu isimame imara
- Msiwasahau wazazi wenu pia
 Kwani hao ndio nguzo ya masha yenu
 Watoto wenu na muwatunze vema
 Muwapeleke kwa kanisa ya Bwana
- Na sisi sote tulioshuhudia
 Arusi yenu siku hii ya leo
 Twawahimiza mheshimu ndoa yenu
 Kwani ndoa ni sakramenti takatifu
 
 Yelele lele, yelele lele
 Shangilieni maharusi hawa, furahieni maharusi hawa