Nimemwacha Wapi Bwana

Nimemwacha Wapi Bwana
Performed by-
CategoryTafakari
ComposerE. A. Minja
Views6,849

Nimemwacha Wapi Bwana Lyrics

  1. Mimi ni kitu gani na niko wapi, ninatoka wapi
    Ninakwenda wapi, mimi nimemwacha Bwana wangu nimtumainiaye
    Kaniumba kanitofautisha na wanyama kwa utashi
    Ndiye anayeitegemeza nafsi yangu mchana usiku hunilinda

    {Nimemwacha wapi (Bwana) Bwana wangu
    mimi naenda kujiongoza
    Imani yangu imekuwa nia tu siku hadi siku
    Matendo yangu yamekuwa ni kinyume toka kitambo
    Kwa ajili hii ona ninafanya kazi
    na kujinyima nafsi yangu mema } *2

  2. Maisha yangu ni safari tangu kuumbwa kuzaliwa
    Na kuishi kwangu hapa duniani mwisho nipate uzima wa milele
    Yeye anipaye pumzi ya uhai wangu na mlinzi wa maisha yangu
    Kwa kila hatua ya maisha yangu hapa duniani
  3. Kanisani nakwenda natoa sadaka na zaka
    Lakini ulevi mimi unanitawala kwani pombe ndiye wangu mfariji
    Anasani maishani yake na ya famili yake
    Na gizani uzinzi ni wangu rafiki sakramenti ya ndoa iko wapi
  4. Watoto wapatao mali kwa mganga kupiga bao
    Nyumba nayo izindikwe hirizi, mikononi nami urogi kaurithi
    Kutosita hio nihoji ndugu na jirani
    Ati jirani yule ndiye jina fulani nikimsema kusengenya napenda
  5. Maana sheria zako ni kama kioo mbele ya matendo yangu,
    Moyo wangu wanielemea nikitafakari matendo yako
    Maana sheria zako ni kama kioo mbele ya imani yangu,
    Maisha yangu yamekuwa gizani tena ni maisha ya dhambi
  6. Ewe ndugu yangu jiulize moyo wako uko wapi
    Na matendo yako yampendeza Muumba wako kwa uzima alokupa
    Ewe Baba mama vijana ewe mlei hebu jiulize
    Mwisho wa maisha yako haya utaupata uzima wa milele