Furaha
| Furaha | |
|---|---|
| Performed by | - | 
| Category | Thanksgiving / Shukrani | 
| Composer | Bernard Mukasa | 
| Views | 6,502 | 
Furaha Lyrics
- Tunakuwa tunasinzia hatujitambui
 Tunaamka tunajikuta tungali haiFuraha furaha furaha furaha
 Bwana Yesu furaha shangwe na chereko
 na furaha, furaha furaha sana
- Mawio mpaka macheo huambatana nasi
 Usiku nguzo ya moto na mchana ya wingu
- Kwenye machozi muda wote tunalia naye
 Anatuinua mkono tukacheka naye
- Tunapoondokewa na ndugu zetu wachache
 Anatupa tumaini kuwapokea kwake
- Tunajivuna kwa sababu tunaye Mungu
 Tunamuomba awe nasi daima milele
Recorded also by St. Don Bosco Kyaani Mombasa
  
 
 
 
  
         
                            