Litukuzeni Jina
   
    
     
         
          
            Litukuzeni Jina Lyrics
 
             
            
- Litukuzeni Jina la Mungu daima milele
 Enyi mataifa, mshangilieni Mungu wetu
 Kwa kuwa Bwana ni Mtukufu wa kutisha
 Yeye ni mfalme mkuu wa dunia yote
 Sifuni Bwana kwa shangwe
 {Jina la Mungu lihimidiwe daima milele
 ( litukuzwe litukuzwe litukuzwe litukuzwe litukuzwe litukuzwe)
 Enyi mataifa mhimidini
 Kwa kuwa fadhili zake (kwetu sisi) zadumu daima milele } *2
- Jina lake Bwana litukuzwe sasa hata milele
 Viumbe vya Bwana Sifuni Bwana Mungu wetu
 Toka mawio hata machweo ya jua
 Sifuni jina lake Bwana Mungu wetu
 Sifuni Bwana Mwenyezi
- Enyi watumishi sifuni Bwana kutoka Mbinguni
 Mbingu nanyi maji, lisifuni jina la Bwana
 Wafalme wa dunia nanyi watu wote
 Wakuu nanyi wakaazi wote wa dunia
 Sifuni Bwana Mwenyezi