Shangilieni Aleluya
   
    
     
         
          
            Shangilieni Aleluya Lyrics
 
             
            
- Shangilieni aleluya,
 Yesu Mkombozi kafufuka
 Amefufuka aleluya,
 tumsherehekee yeye mzima
- Tumwimbie kwa furaha kubwa,
 kwani kaburini ametoka
 Kashinda kifo aleluya,
 aleluya Yesu ni mzima
- Amefufuka Mkombozi,
 aleluya tushangilie
 Nguvu za mwovu ameshida,
 ametuondoa kufani
- Malaika aliwaambia
 wanawake msiogope
 Sasa kaburi liko tupu,
 kwani Yesu amefufuka
- Amebatilisha Shetani,
 amewaletea wokovu,
 Kwani hiyo ninyi mtangaze
 ni hakika Yesu yu hai
- Na sisi sote tumtukuze ,
 Yesu Kristu amefufuka
 Tumwimbieni aleluya,
 siku tatu kafufuka,