Kwa Sherehe na Shukrani

Kwa Sherehe na Shukrani
Performed by-
CategoryPasaka (Easter)
Views3,114

Kwa Sherehe na Shukrani Lyrics

  1. Kwa sherehe na shukrani ya moyo,
    wakristu leo tufanye shangwe
    Tumwimbie Mwokozi siku hiyo,
    amefufuka tufurahiwe

    Amefufuka asifiwe,
    tukaokoke kwa ufufuko we

  2. Maria Salome na Magdalene
    kaburini wenda alfajiri
    Nayo manukato na manemane
    kumtia Yesu kama desturi
  3. Mlangoni mwa kaburi wakifika,
    walikuta ndani yake wazi
    Waambiwa mara na malaika,
    hamo amefufuka Mkombozi
  4. Yesu u mfano wangu maishani,
    nipendelee utakatifu
    Nitatoka nami mzima kaburini,
    nitafufuka mwenye utukufu