Rabi Yesu ni Mzima
   
    
     
         
          
            Rabi Yesu ni Mzima Lyrics
 
             
            
- Rabi Yesu ni mzima leo na mapema akafufuka mzima
 Rabi Yesu ni mzima si kaburini ni salama
 Dhambini haoni, tu maskini, tu utumwani
 Katuokoa motoni mwovu shetani mtafuta shani
 Adui kashindwa haponi
- Za Rabi zetu nyimbo, twatia mapambo tusifu mambo
 Za Rabi zetu nyimbo, ya shetani huvunja mitambo
 
 Msalabani we, tuokolowe, Mungu mwenyewe
 Hanyimi afungiwe, nasi wenyewe na moyo tuwe
 haya tufuate mfanowe
- Rabi mshangilieni, watu wa imani, ndugu zangu karibuni,
 Rabi Mshangilieni, ameshinda msiche shetani
 
 Nasi hakika hapana shaka, tutafufuka
 kaburi tutatoka, na malaika kuhesabika
 Wema wa Mungu katuzika
- Mkate ukigeuka, Rabi atashuka, nyoyo zetu kutaka
 Mkate ukigeuka, heshima twende kupeleka,
 
 Na ninyi tena, taabu mkiona jueni vyema, leo raha hakuna
 Tupande sana, kesho kuvuna,
 milele na Rabi kuonana