Rabi Yesu ni Mzima

Rabi Yesu ni Mzima
Performed by-
CategoryPasaka (Easter)
Views3,179

Rabi Yesu ni Mzima Lyrics

  1. Rabi Yesu ni mzima leo na mapema akafufuka mzima
    Rabi Yesu ni mzima si kaburini ni salama

    Dhambini haoni, tu maskini, tu utumwani
    Katuokoa motoni mwovu shetani mtafuta shani
    Adui kashindwa haponi

  2. Za Rabi zetu nyimbo, twatia mapambo tusifu mambo
    Za Rabi zetu nyimbo, ya shetani huvunja mitambo

    Msalabani we, tuokolowe, Mungu mwenyewe
    Hanyimi afungiwe, nasi wenyewe na moyo tuwe
    haya tufuate mfanowe
  3. Rabi mshangilieni, watu wa imani, ndugu zangu karibuni,
    Rabi Mshangilieni, ameshinda msiche shetani

    Nasi hakika hapana shaka, tutafufuka
    kaburi tutatoka, na malaika kuhesabika
    Wema wa Mungu katuzika
  4. Mkate ukigeuka, Rabi atashuka, nyoyo zetu kutaka
    Mkate ukigeuka, heshima twende kupeleka,

    Na ninyi tena, taabu mkiona jueni vyema, leo raha hakuna
    Tupande sana, kesho kuvuna,
    milele na Rabi kuonana