Leo ni Siku ya Pasaka
   
    
     
         
          
            Leo ni Siku ya Pasaka Lyrics
 
             
            
- Leo ni siku ya Pasaka, tumshangilie Bwana wetu -
 Leo ni siku ya Pasaka, tumshangilie Bwana wetu
 Mwanakondoo aliyekufa atawala mzima leo
 
 Aleluya Bwana Yesu leo ameshinda kifo *2
 Aleluya Bwana Yesu leo amshinda kifo *2
 Yesu tumaini (letu) kafufuka mfalme (wetu)
 Sote na tuimbe, (hosanna) tukimsifu Mfalme (wetu)
 Aleluya Bwana Yesu leo ameshinda kifo
- Kristu mshindaji wetu atupatanisha na Baba
 Katika wafu ametoka tumshangilie Bwana wetu
- Maria Magdalena tuambie ni nini ulichoona leo
 Niliona kaburi tupu sanda na nguo zimebaki
 nikawaona malaika wakitangaza ufufuko
 
 Niliona kaburi tupu sanda na nguo zimebaki
 nikawaona malaika wakitangaza ufufuko
 
 Sasa nasi tuombe atusaidie tushinde pia
 Kristu uliyefufuka utuhurumie na sisi
 
 Kristu uliyefufuka utuhurumie na sisi