Leo ni Siku ya Pasaka

Leo ni Siku ya Pasaka
Performed by-
CategoryPasaka (Easter)
Views3,198

Leo ni Siku ya Pasaka Lyrics

  1. Leo ni siku ya Pasaka, tumshangilie Bwana wetu -
    Leo ni siku ya Pasaka, tumshangilie Bwana wetu
    Mwanakondoo aliyekufa atawala mzima leo

    Aleluya Bwana Yesu leo ameshinda kifo *2
    Aleluya Bwana Yesu leo amshinda kifo *2
    Yesu tumaini (letu) kafufuka mfalme (wetu)
    Sote na tuimbe, (hosanna) tukimsifu Mfalme (wetu)
    Aleluya Bwana Yesu leo ameshinda kifo
  2. Kristu mshindaji wetu atupatanisha na Baba
    Katika wafu ametoka tumshangilie Bwana wetu
  3. Maria Magdalena tuambie ni nini ulichoona leo
    Niliona kaburi tupu sanda na nguo zimebaki
    nikawaona malaika wakitangaza ufufuko

    Niliona kaburi tupu sanda na nguo zimebaki
    nikawaona malaika wakitangaza ufufuko

    Sasa nasi tuombe atusaidie tushinde pia
    Kristu uliyefufuka utuhurumie na sisi

    Kristu uliyefufuka utuhurumie na sisi