Uzuio wa Umeme

Uzuio wa Umeme
Performed by-
CategoryTafakari
Views2,124

Uzuio wa Umeme Lyrics

  1. Uzuio wa umeme, mlinzi wa Kimasai
    Mbwa mkali tunguri na silaha za kisasa
    hakika, hazifai kitu, kweli hazifai kitu
    Bwana amtumapo mjumbe kuchukua roho yako

  2. Wako wapi, wako wapi waliowahi kutikisa dunia?
    Wako wapi walioita miungu na dunia?
    Na hakuna hata mmoja wao aliyewahi kujikinga
    Bwana alipomtuma mjumbe kumchukua?
  3. Wako wapi, wako wapi waliowahi kuishi angani?
    Wako walio ishi kwenye madaha?
    Je hakuna hata mmoja wao aliyeweza kujificha
    Bwana alipomtuma mjumbe kumchukua