Tumshangilie Maria

Tumshangilie Maria
Performed by-
AlbumUwe Nasi Mama Maria
CategoryBikira Maria
Views6,181

Tumshangilie Maria Lyrics

  1. Ni Maria mtakatifu, tumshangilie Maria
    Ni mzazi wa Mungu Mwana
    Ni mkuu wa mabikira
    Ni mama yake Yesu Kristu

    Vigelegele vifijo na makofi
    Hoye hoye nderemo nyingi
    Pia vifijo tumshangilie Mama Maria
    Yeye ni mwombezi wetu na msaada
    Njooni tumwimbie chereko mama

  2. Mama wa neema ya Mungu -
    Mama mtakatifu sana -
    Mama wa usafi wa moyo -
    Mama usiye na doa -
  3. Ni mama usiye na dhambi
    Pia mama mpendelevu
    Ni mama msaada wetu
    Ni mama wa shauri jema
  4. Ni Mama wa Muumba wetu
    Pia mama wa Mkombozi
    Bikira wa utaratibu
    Ni bikira mwenye heshima
  5. Ndiye bikira mwenye sifa
    Ndiye bikira mwenye enzi
    Ni bikira mwenye huruma
    Na ndiye bikira amini
  6. Na ndiye kioo cha haki
    Ni kikao chenye heshima
    Sababu ya furaha yetu
    Ndiye chombo chenye rehema
  7. Ndiye chombo chenye heshima
    Ni chombo chema cha ibada
    Ndiye waridi lenye fumbo
    Ndiye manara wa Daudi
  8. Yeye ni mnara wa pembe
    yeye ni nyumba ya dhahabu
    Ndiye sanduku la agano
    Yeye ni mlango wa mbingu
  9. Ndiye nyota ya asubuhi
    Yeye ni afya ya wagonjwa
    Kimbilio la wakosefu
    Mfariji wa wenye uchungu
  10. Ni msaada wa Wakristu
    Malkia wa malaika
    Ndiye malkia wa mababu
    malkia wa manabii
  11. Ndiye malkia wa mitume
    Malkia wa mashahidi
    Malkia wa waungama
    Malkia wa mabikira
  12. Malkia wa watakatifu
    Aliyepalizwa mbinguni
    Ni wa Rosari takatifu
    Ndiye Malkia wa amani