Kwa Nini Wasimama Mbali
| Kwa Nini Wasimama Mbali | |
|---|---|
|  | |
| Performed by | St. Maurus Kurasini | 
| Album | Hubirini Kwa Kuimba | 
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) | 
| Composer | D. Mlolwa | 
| Video | Watch on YouTube | 
| Views | 16,099 | 
Kwa Nini Wasimama Mbali Lyrics
- Bwana ee Bwana, kwa nini wasimama mbali
 Ee Bwana ee Bwana, kwa nini wasimama mbali
 { Kwa nini kujificha na kujificha nyakati za shida
 Kwa nini kujificha Bwana nyakati za shida } *2
- Kwa kiburi chake mtu asiye haki
 Mnyonge anafuatiwa anafuatiwa kwa ukali
 Na wanaswe kwa hila hizo hizo walizoziwaza
- Maana mdhalimu, mdhalimu hujisifia
 Hujisifia sifia tamaa ya nafsi yake
 Na mwenye uchoyo humkataa Bwana na kumdharau
- Asema moyoni mwake, asema sitaondoshwa
 Kizazi hata kizazi, sitakuwamo taabuni
 Kinywa chake kimejaa laana na hila na dhuluma
 
  
         
                            