Kwa Nini Wasimama Mbali
| Kwa Nini Wasimama Mbali | |
|---|---|
![]() | |
| Performed by | St. Maurus Kurasini |
| Album | Hubirini Kwa Kuimba |
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) |
| Composer | D. Mlolwa |
| Video | Watch on YouTube |
| Views | 16,206 |
Kwa Nini Wasimama Mbali Lyrics
Bwana ee Bwana, kwa nini wasimama mbali
Ee Bwana ee Bwana, kwa nini wasimama mbali
{ Kwa nini kujificha na kujificha nyakati za shida
Kwa nini kujificha Bwana nyakati za shida } *2- Kwa kiburi chake mtu asiye haki
Mnyonge anafuatiwa anafuatiwa kwa ukali
Na wanaswe kwa hila hizo hizo walizoziwaza - Maana mdhalimu, mdhalimu hujisifia
Hujisifia sifia tamaa ya nafsi yake
Na mwenye uchoyo humkataa Bwana na kumdharau - Asema moyoni mwake, asema sitaondoshwa
Kizazi hata kizazi, sitakuwamo taabuni
Kinywa chake kimejaa laana na hila na dhuluma
