Njooni Tushukuru
   
    
     
         
          
            Njooni Tushukuru Lyrics
 
             
            
- Watu wote njooni tushukuru, njooni tushukuru aee,
 Simameni tuseme asante, tuseme asante aee
 {Na tuimbe - kwa vigelegele
 Na tucheze - ngoma na vinanda
 Kwa vinubi, zeze na filimbi aee } *2
- Yeye ndiye aliyeziumba, mbingu na dunia aee
 Vitu vyote vionekanavyo, na visivyoonekana
- Kwa mfano wake katuumba, tufanane naye aee
 Ametupa vyote tutawale, tumtumikie aee
- Shukuruni Mungu wa miungu, Bwana wa mabwana aee
 Zitoeni dhabihu za shangwe, za kumshukuru aee
- Tukuzeni Mungu siku zote, daima milele aee
 Msifuni kwa kila sauti hata kwa ukimya aee