Bwana Nikufananishe Na Nini

Bwana Nikufananishe Na Nini
Performed bySt. Cecilia Kijenge
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerDeo Kalolela
Views9,446

Bwana Nikufananishe Na Nini Lyrics

  1. Bwana nikufananishe na nini
    Au nikufananishe na nani
    Pendo lako Bwana ni la ajabu
    Ndiyo sababu ya furaha yangu

  2. Kwa kuwa Bwana ulinijua
    Tangu tumboni mwa mama yangu
    Ukanitunza kwa upendo
    Ukanijaza pendo lako
  3. Nilipokuwa kwenye mateso
    Nilifikiri umeniacha
    Mawazo yangu ya kitoto
    Sikutambua pendo lako
  4. Kwangu ulijifunua Bwana
    Moyo wangu ulikutambua
    Matendo mengi yenye nguvu
    Uliyotenda mbele yangu