Ndiwe Sitara Yangu
   
    
     
         
          
            Ndiwe Sitara Yangu Lyrics
 
             
            
- {Ndiwe sitara yangu Bwana
 Utanihifadhi na mateso
 Utanizungusha nyimbo za wokovu
 Nyimbo za wokovu } *2
- Nalia mchana kutwa, nalia usiku kucha
 Lakini nafuu sipati Bwana usinitupe
- Bwana ni mdudu, wala si mtu kabisa
 Nimepuuzwa na kudharauliwa na kila mtu
- Ulimi wangu wang'ata kinywani mwangu ee Bwana
 Umeniacha kama mpumbavu mimi ninaangamia
- Bwana wewe ulitoa, Bwana wewe umetwaa
 Nichukue nami nikapumzike pema peponi
- Atukuzwe Mungu Baba, na mwanaye mtukuka
 Atukuzwe na Roho Mtakatifu milele amina