Mungu Wangu Mbona Umeniacha
| Mungu Wangu Mbona Umeniacha | |
|---|---|
| Performed by | St. Maurus Kurasini | 
| Album | Hubirini Kwa Kuimba | 
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) | 
| Composer | G. A Chavalla | 
| Views | 41,977 | 
Mungu Wangu Mbona Umeniacha Lyrics
- Mungu wangu mbona umeniacha mimi
 Katika taabu zote hizi
 Maisha yangu ni ya mashaka
 Kwani sina raha nimekosa amani
 Matatizo mengi yananisonga (sana)
 Nakuomba Bwana nisaidie
 Maadui zangu wananiwinda (kutwa)
 Wanitega ili wanikamate
 Ninalala macho wazi mimi (kama ndege)
 Kama ndege mkiwa juu ya paa
 Nimekuwa kama mhuni mimi (fanya hima)
 Fanya hima Bwana kuniokoa
- Nimekuwa kama kichekesho kwa watu jamani mimi Bwana
 Kila nipitapo hunisema na kunicheka
 Wananizushia maneno ya uongo jamani mimi Bwana
 Mimi nimekuwa ni jalala la kila baya
- Maadui zangu kutwa wanisimanga jamani mimi Bwana
 Wananidhihaki wanisonya na kunitusi
 Jina langu limekuwa gumzo lao jamani mimi Bwana
 Sasa ndilo walitumialo kwa kulaania
- Na majivu yamekuwa chakula changu jamani mimi Bwana
 Na machozi yangu yamekuwa kinywaji changu
 Na siku zangu zinapita kama moshi jamani mimi Bwana
 Nakuomba usinichukue bado kijana
 
  
         
                            