Matumaini ya Safari

Matumaini ya Safari
Performed by-
AlbumMatumaini ya Safari
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
ComposerMarcus Mtinga
Views9,413

Matumaini ya Safari Lyrics

  1. Matumaini ya safari yetu, sasa yameingia dosari
    Kwani meli tuliyopanda, kuja kwako,
    Tazama imevamiwa na majambazi
    Hatuna njia nyingine itakayotuokoa kwenye janga hili
    Yesu mwema njoo haraka, utuokoe wanao tunakwisha wote
  2. Gonjwa hatari, lisilotibika, ona linatumaliza wote
    Halichagui halibagui, linafyeka,
    Ukimwi, halina huruma kwa wanadamu
    Limeua watu wengi, ni wengi wakubwa kwa wadogo wamepotea
    Milenia tuliyomaliza, ilijaa huzuni na majonzi kila upande
  3. Wanasayansi madaktari, wanaahangaika kutwa kucha
    Juhudi zinagonga mwamba, hakuna dawa
    Ee Bwana tunakufa tuonee huruma
    Tunaomba Mungu Mwenyezi, ingilia katika uwezo wako wote
    Macho yao uyafumbue, fanaka ipatikane, Bwana tunakuomba
  4. Tumeshaomba, tumesali sana, ee Bwana sikia sala zetu
    Tunaungama tumekosa Mungu Mwenyezi,
    tazama, Tunakulilia tusikilize
    Tunakufa kama nzige, ee Mungu ee Bwana tunateketea wote
    Si Sodoma wala Gomora, jamani hili linazidi tena latisha
  5. Ee Yesu Mwema, mwenye huruma, tunakuomba ututazame
    Damu na maji vilivyotoka mwilini mwako
    Zilete dawa halisi ya kutuponya
    Watoto ni wengi sana wanakufa bila ya hatia, inasikitisha
    Wengine sasa ni yatima, hawajui wataishi vipi maisha yao
  6. Tunakuomba, ee Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu
    Milenia tuliyoianza, njoo Bwana,
    Haraka ukatawale mioyo yetu
    Machozi tunayolia yafute maovu yetu yote kwa neema yako
    Lakini mapenzi yako yatimizwe vile utakavyotuashiria