Yu Mwangu kweli Mungu

Yu Mwangu kweli Mungu
Performed by-
CategoryTBA
Composer(traditional)
Views1,433

Yu Mwangu kweli Mungu Lyrics

  1. Yu mwangu kweli Mungu a, yu nami si uongo,
    Naye mamoja nangu a, niliye mdude mdogo,
    Ee Rabbi nakuungama, ndiwe mkombozi wangu
    Mwenyezi, mwenezi, mtoaji wa neema
    Mwenyezi, mwenezi, mtoaji wa neema
  2. Na haya kwani mdhambi mno, nawe mtukufu
    Ee mambo yasiyo mfano, mpenda utakatifu
    Nakuabudu mi mjao, tayari masikanio
    Kwenenda, kutenda, kwa kila amriyo
    Kwenenda, kutenda, kwa kila amriyo
  3. Walakini mi mdhaifu, kusema sikufanya
    Hivyo nilivyo mkosefu, hata naona haya
    Ee Rabbi wezesha moyo, wangu hutia neemayo
    Utake, ushike, yote mapenziyo
    Utake, ushike, yote mapenziyo