Alidharauliwa na Kukataliwa

Alidharauliwa na Kukataliwa
Performed by-
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
ComposerMartin M. Munywoki
Views4,458

Alidharauliwa na Kukataliwa Lyrics

  1. Alidharauliwa na kukataliwa kukataliwa na watu
    Mtu mwenye huzuni nyingi ajuaye sikitiko

  2. Alikua mbele zake kama mche mwororo,
    Na kama mzizi katika nchi nchi kavu
    Hakuwa na umbo kuvutia wala uzuri,
    Hata tumwonapo tumtamani
    Ni kama mtu ambaye watu humficha uso,
    Wala hatukumhesabia kuwa kitu
  3. Hakika amechukua masikitiko yetu,
    Amejitwika huzuni zetu amejitwika.
    Lakini na sisi tulidhani kuwa kapigwa,
    Amepigwa na Mungu na kuteswa
    Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu,
    Alichubuliwa kwa maovu maovu yetu
  4. Adhabu ya amani yetu ilikuwa kwake,
    Na kwa kupigwa kwake yeye sisi tumepona
    Sisi sote kama ko-ndoo tumepotea,
    Kila mmoja njia yake yeye,
    Bwana ameweka juu yake maovu yetu,
    Alione-wa lakini alinyenyekea
  5. Alionewa lakini hakufunua kinywa,
    Kama mwanakondoo akipelekwa machinjoni
    Kwa kuonewa kuhukumiwa kaondolewa,
    ni nani atasimulia haya?
    Ni nani aliyesadiki habari hii?
    na mkono wa Bwana amefunuiwa nani?