Watikisa Kibuyu

Watikisa Kibuyu
Performed bySame KMJ
AlbumWatikisa Kibuyu
CategoryTafakari
ComposerE. A. Minja
Views9,516

Watikisa Kibuyu Lyrics

  1. Nini siri ya moyo wako kupenda kuwa mtu wa roho mbaya?
    Daima moyo wako wasononeka kwa kujiuliza kwa nini?
    Jirani yako anapofanikiwa moyo wako wakosa raha
    Si zuri si jema moyo wako wakutesa ukiwaza kwa nini!

    Na tazama sasa- unachokifanya,
    Ni kukimbilia - kutikisa kibuyu
    Na imani yako - ni kwenye kibuyu na kibuyu ndiye mungu wako

  2. Wengine wanakiita ni kinga na kukifanya kama mungu wao
    Na tena jina jingine ni 'kimo' sababu yake na kiza ni wivu
    Unajisifia ni mtu mwema mwenye roho iliyo na huruma
    Lakini kwa ndani wewe mbaya roho imetawaliwa na wivu!
    Ukirudi kazi kwako ni moja kukitikisa tikisa kibuyu!
    Ah! kumbe waroga umejawa na imani chafu!
  3. Mtoto wa jirani kafaulu katika kazi au ni masomo
    Ukijua wakiwaza kibuyu ugeuze miguu yake nyuma
    Wenzako wanaongeza bidii ya kujituma kwenye kazi zao
    Wewe unawatazama vibaya na kuanza kukiwaza kibuyu
    Ukirudi kazi kwako ni moja kukitikisa tikisa kibuyu
    Ah! kumbe waroga umejawa na imani chafu
  4. Unapomtazama ndugu yako kajenga nyumba na inapendeza
    Ukiitazama moyo wauma sasa wawaza huyu asiishi!
    Ukirudi kazi kwako ni moja kukitikisa tikisa kibuyu!
    Ah! kumbe waroga umejawa na imani chafu!
  5. Sasa jifikirie ndugu wewe badili roho yako yenye wivu
    Na kuutengeneza moyo wako ukafanane nao malaika
    Ukirudi kazi kwako ni moja ni kupiga magoti na kusali
    Ah! Kumbe waomba upendo uwepo duniani