Maneno Saba ya Yesu Msalabani

Maneno Saba ya Yesu Msalabani
Performed by-
AlbumMtazame Mkombozi Msalabani
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
ComposerE. Z. Ng
Views14,373

Maneno Saba ya Yesu Msalabani Lyrics

  1. Baada ya kuteswa na kusulubiwshwa msalabani
    Aliona walichokifanya hawakukijua
    Aliwaombea kwa Mungu akisema
    Baba uwasamehe hawalijui wanalofanya
  2. Kulikuwa mhalifu liyemtambua kuwa yeye ni Mungu
    Alitubu akaambiwa
    Nakuambia hakika leo, utakuwa pamoja nami peponi
  3. Alitukabidhi kwa mama yake
    Na huyo ndiyo mwombezi wetu aliposema
    Mama tazama huyu ndiye mwanao
    Tazama huyu ndiye mamako
  4. Aliona kiu baada ya mateso makali
    Hadi alisema mwenyewe naona kiu
  5. Baada ya mateso makali hayo
    Aliyoteswa kwa ajili ya dhambi zetu
    Aliona yote aliyotumwa na Mungu kuwa yametimia
    Aliposema Yametimia *2
  6. Ndipo alipolia kwa uchungu na kumbwambia Baba
    Eloi eloi lamasabakidani, Mungu wangu Mbona umeniacha
  7. Mwisho kabisa aliikabidhi roho yake kwa Baba
    Akisema Baba mikononi mwako Naiweka Roho yangu