Maneno Saba ya Yesu Msalabani
| Maneno Saba ya Yesu Msalabani | |
|---|---|
| Performed by | - | 
| Album | Mtazame Mkombozi Msalabani | 
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) | 
| Composer | E. Z. Ng | 
| Views | 17,783 | 
Maneno Saba ya Yesu Msalabani Lyrics
- Baada ya kuteswa na kusulubiwshwa msalabani
 Aliona walichokifanya hawakukijua
 Aliwaombea kwa Mungu akisema
 Baba uwasamehe hawalijui wanalofanya
- Kulikuwa mhalifu liyemtambua kuwa yeye ni Mungu
 Alitubu akaambiwa
 Nakuambia hakika leo, utakuwa pamoja nami peponi
- Alitukabidhi kwa mama yake
 Na huyo ndiyo mwombezi wetu aliposema
 Mama tazama huyu ndiye mwanao
 Tazama huyu ndiye mamako
- Aliona kiu baada ya mateso makali
 Hadi alisema mwenyewe naona kiu
- Baada ya mateso makali hayo
 Aliyoteswa kwa ajili ya dhambi zetu
 Aliona yote aliyotumwa na Mungu kuwa yametimia
 Aliposema Yametimia *2
- Ndipo alipolia kwa uchungu na kumbwambia Baba
 Eloi eloi lamasabakidani, Mungu wangu Mbona umeniacha
- Mwisho kabisa aliikabidhi roho yake kwa Baba
 Akisema Baba mikononi mwako Naiweka Roho yangu
 
  
         
                            