Njia za Mkato

Njia za Mkato
Performed by-
CategoryTafakari
ComposerMartin M. Munywoki
Views3,028

Njia za Mkato Lyrics

  1. // utangulizi //
    Haraka hara-ka haina baraka,
    (ndugu yangu) ka-wia ufike uendapo salama
    Jifunze subi-ra na uvumilivu,
    (fanya kazi) usipende kupata vya rahisi vya bure
    Haupendi kuchoka - wala kutoa jasho
    Wategemea - mali ya ndugu yako
    Haupendi kungoja - wala kuulizia
    Unafuata - njia za vichochoro!

    // kiitikio //

    Njia za mkato ee -
    Njia za mkato ee ni hatari sana
    Zenye mabonde na maporomoko ee-
    Na maporomoko ee ni hatari sana
    Hizo za vichochoro ee-
    Za vichochoroni ee ni hatari sana
    Humo wamejaa na wanyang'anyi ee-
    Nao wanyang'anyi ee ni hatari sana jihadhari sana


    // mashairi //
  2. Mbona unataka mali upesi pasipo kutoa jasho
    Vijia vya mkato unavipenda
    Unaiba wala rushwa unavuna usikopanda
    Majibu ya haraka unayapenda
  3. Mbona unafurahia uzinzi pasipo kufunga ndoa
    Vijia vya mkato unavipenda
    Unapolemewa na ndoa wamkimbilia mganga
    Majibu ya haraka unayapenda
  4. Mbona unapokosea wewe wajitetea kwa uongo
    Vijia vya mkato unavipenda
    Unapokosana na ndugu wasuluhisha kwa vita
    Majibu ya haraka unayapenda