Nashukuru Bwana

Nashukuru Bwana
Performed by-
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerStanslaus Mujwahuki
Views5,668

Nashukuru Bwana Lyrics

  1. Nashukuru Bwana, ee Bwana nashukuru sana
    Kwa yote yote, uliyonijalia mimi kiumbe chako,
    Niliye mdogo mbele yako
    Nitaimba sifa zako ooo milele na milele

  2. Siku zote, Bwana wanipa mkate
    Japo kidogo, silali njaa, hata siku moja
  3. Shamba langu, nimepanda nimepata,
    Mazao mengi, yapo ghalani, ghalani mwangu
  4. Unanipa, nguvu za kuwashinda
    Wanaoniwinda, mwili na roho, wanimalize
  5. Bila wewe, mimi siwezi kitu,
    Vitu vyote, nilivyo navyo, nimepata kwako
  6. Wema wako, kwangu mimi mwanao,
    Haupimiki, nashukuru Bwana, nashukuru Bwana