Tu Mavumbi Sisi
| Tu Mavumbi Sisi | |
|---|---|
| Performed by | Kwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha | 
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) | 
| Views | 12,971 | 
Tu Mavumbi Sisi Lyrics
- { Siku zinapita, miaka yapita
 Neno lake Bwana halitapita kamwe }*2
- Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini *2
- mmmm mmmm mmm siku hiyo ni ya huzuni mno
 mmmm mmmm mmm siku hiyo kweli inatisha
- Kwa maana siku hiyo,
 Mavazi yako yatakuwa ni sanda
 Kitanda chako kitakuwa jeneza
 Na nyumba yako iyakuwa kaburi
 Jamaa zako watakutupia udongo,
 kwa heri ya milele!
- Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini *2
- { Roho ndiyo roho ndiyo itiayo uzima
 Mwili haufai kitu } * 2
- Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini
- Tazameni mimea, shambani
 Matunda na maua, vyapendeza
 Vyote vitanyauka
 Wanyama wa pori, na nyumbani
 Na ndege angani, wapendeza
 Wote wataangamia
- Ee ndugu sasa utubu rudi
 Mrudie Mungu wako
 Kwa maana duniani sisi ni wasafiri
 Hujui saa na siku ndugu ya kuiacha dunia
 Kwa maana duniani sisi ni wasafiri
- Sayari angani zapendeza
 Mito na mabonde duniani
 Vyote vitatokomea
 Mungu ndiye peke ajuaye
 Siri ya maisha ya viumbe
 Vyake ulimwenguni
- { Siku zinapita, miaka yapita
 Neno lake Bwana halitapita kamwe }*2
 Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini * 2
 
  
         
                            