Tazama Mama Mwanao

Tazama Mama Mwanao
Performed bySt. Patrick Morogoro
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
Views3,715

Tazama Mama Mwanao Lyrics

  1. Tazama Mama mwanao, atundikwa msalabani
    Sababu gani hi-yo, mwanao kutiwa hatiani
    { Uchungu, mama, uchung,u mama,
    Uchungu mama kwa mwanao } *2

  2. [ s ] Sioni kosa lolote, alilolitenda mwanangu
    Mwanangu hakuwa na kosa, makosa hayo juu yenu
    Uchungu, uchungu, uchungu sana kwa mwanangu *2
  3. [ t ] Kutundikwa juu msalabani, sababu yake ukombozi
    Atukomboe utumwani, tuwe wana wa ukombozi
    Ni sisi, ni sisi, ni sisi mama wakosefu *2
  4. [ s ] Mwanangu haikumpasa, kufa bure bila sababu
    Mwanangu Mungu mtu pekee, kwake sioni kosa kwangu
    Uchungu, uchungu, uchungu sana kwa mwanangu *2
  5. [ t ] Kumbuka mama Maria, maneno ya mwanao Yesu
    Nitakufa nitafufuka, na kwenda juu kwa Baba yangu
    Ya nini, ya nini, ya nini mama huzuni hiyo