Misa Subukia

Misa Subukia
Performed by-
CategoryMisa (Sung Mass)
Views63,086

Misa Subukia Lyrics

BWANA BWANA UTUHURUMIE

  1. Bwana, Bwana, Bwana utuhurumie *2
  2. Kristu utuhurumie, Kristu utuhurumie *2
  3. Bwana, Bwana, Bwana utuhurumie *2

UTUKUFU JUU KWA MUNGU (SUBUKIA)

  1. { Utukufu juu kwa Mungu, na amani duniani,
    kwao watu wenye mapenzi,
    watu wenye mapenzi mema } *2

  2. Tunakusifu tunakuheshimu, twakuabudu tunakutukuza
    Twakushukuru kwa ajili yako, ya utukufu wako mkuu.
  3. Ee Mungu baba ndiwe mfalme,
    Mfalme wa Mbinguni baba mwenyezi.
    Ee Yesu Kristu mwana wa pekee,
    mwanakondoo mwana wa Baba.
  4. Uondoaye dhambi za watu tuhurumie tusikilize,
    Tuhurumie mwenye rehema maombi yetu uyapokee.
  5. Uketiye kuume kwake, Mungu baba tuhurumie.
    Kwa kuwa ndiwe pekee yako, Pekee yako Mtakatifu.
  6. Pamoja naye roho Mtakatifu, katika utukufu wake
    Anayeishi na kutawala, milele yote Amina.

MTAKATIFU (SUBUKIA)

  • Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu Mungu wa majeshi
    Mbingu na dunia zimejaa, zimejaa utukufu wako.
  • Hosanna hosanna hosanna hosanna juu mbinguni
  • Mbarikiwa anayekuja anayekuja kwa Jina la Bwana