Enyi Wakristu Wapenzi
Enyi Wakristu Wapenzi Lyrics
{ Enyi wakristu wapenzi njooni
Bwana anatualika kwenye karamu } *2
Kwanza ndugu tazama meza yake inavyopendeza
Yeye Bwana na wateule wameizunguka meza yake
Haya ndugu simama nawe ushiriki *2
- Njoni Bwana atuita meza yake sasa itayari
Haya simama nenda nawe ushiriki
- Kama wewe wastahili fanya hima ukampokee
Ndicho chakula chenye uzima milele
- Yeye anilaye mimi atakuwa na uzima mpya
Siku ya mwisho mimi nitamfufua
- Yeye katuandalia masikini pia matajiri
Ukarimu gani Bwana Yesu alionao