Msisimko wa Sifa
| Msisimko wa Sifa | |
|---|---|
|  | |
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Asifiwe Bwana Mungu (Vol 8) | 
| Category | Thanksgiving / Shukrani | 
| Composer | J. C. Shomaly | 
| Video | Watch on YouTube | 
| Views | 8,760 | 
Msisimko wa Sifa Lyrics
- Tunayapiga makofi na nyimbo za sifa,
 Tunashangilia, tunafurahia
 Leo tunasisimka kumshukuru MuumbaHuo - ndio kweli, msisimko wa si-fa kweli
 Pepo - na shetani wameshatimua mbi-o kweli
 Tuna-lipa sifa jina lake Yesu Kri-stu kweli
 Nasi - twamsifu Mungu kwa shangwe na si-fa
 { Sisimka (sisimka) sisimka (sasa sisimka)
 Shangilia (tuimbe wote) Jina Yesu
 Tumeuona wema wake na mkono wake umetubariki } *2
- Jua linapochomoza jogoo kawika,
 Mungu katupenda, anatuamsha
 Leo tunasisimka kumshukuru Muumba
- Mvua nayo inanyesha sisi hatujui,
 Imetoka wapi, mapenzi ya Mungu
 Leo tunasisimka kumshukuru Muumba
- Vyakula tunavyokula vinatupa nguvu,
 Twatembea vyema, na akili nyingi
 Leo tunasisimka kumshukuru Muumba
- Majira nazo nyakati azipanga Mungu,
 Sisi tunaishi, kwa mapenzi yake
 Leo tunasisimka kumshukuru Muumba
 
  
         
                            