Msisimko wa Sifa

Msisimko wa Sifa
Performed bySt. Paul Students' Choir (University of Nairobi)
AlbumAsifiwe Bwana Mungu (Vol 8)
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerJ. C. Shomaly
VideoWatch on YouTube
Views7,701

Msisimko wa Sifa Lyrics

  1. Tunayapiga makofi na nyimbo za sifa,
    Tunashangilia, tunafurahia
    Leo tunasisimka kumshukuru Muumba

    Huo - ndio kweli, msisimko wa si-fa kweli
    Pepo - na shetani wameshatimua mbi-o kweli
    Tuna-lipa sifa jina lake Yesu Kri-stu kweli
    Nasi - twamsifu Mungu kwa shangwe na si-fa
    { Sisimka (sisimka) sisimka (sasa sisimka)
    Shangilia (tuimbe wote) Jina Yesu
    Tumeuona wema wake na mkono wake umetubariki } *2

  2. Jua linapochomoza jogoo kawika,
    Mungu katupenda, anatuamsha
    Leo tunasisimka kumshukuru Muumba
  3. Mvua nayo inanyesha sisi hatujui,
    Imetoka wapi, mapenzi ya Mungu
    Leo tunasisimka kumshukuru Muumba
  4. Vyakula tunavyokula vinatupa nguvu,
    Twatembea vyema, na akili nyingi
    Leo tunasisimka kumshukuru Muumba
  5. Majira nazo nyakati azipanga Mungu,
    Sisi tunaishi, kwa mapenzi yake
    Leo tunasisimka kumshukuru Muumba