Mshukuruni Bwana
Mshukuruni Bwana | |
---|---|
Choir | St. Cecilia Mwenge Dsm |
Category | Thanksgiving / Shukrani |
Composer | P. F. Mwarabu |
Reference | Ps. 136 |
Mshukuruni Bwana Lyrics
{ Mshukuruni Bwana, Mshukuruni Bwana Mungu
kwa kuwa ni mwema
Kwa maana fadhili zake ni za milele } *2
-
Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya Bwana,
Kuzihubiri sifa zake zote -
Akaikemea bahari ya shamu ikakauka
Akawaongoza vilindini kana kwamba ni mchanga -
Akawaokoa na mkono wa mtu aliyewachukia
Na kuwakomboa na mkono wa adui zao -
Maji yakawafunika watesi wao
Hakusalia hata mmoja wao