Mshukuruni Bwana

Mshukuruni Bwana
Performed bySt. Cecilia Mwenge Dsm
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerP. F. Mwarabu
Views4,172

Mshukuruni Bwana Lyrics

  1. { Mshukuruni Bwana, Mshukuruni Bwana Mungu
    kwa kuwa ni mwema
    Kwa maana fadhili zake ni za milele } *2

  2. Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya Bwana,
    Kuzihubiri sifa zake zote
  3. Akaikemea bahari ya shamu ikakauka
    Akawaongoza vilindini kana kwamba ni mchanga
  4. Akawaokoa na mkono wa mtu aliyewachukia
    Na kuwakomboa na mkono wa adui zao
  5. Maji yakawafunika watesi wao
    Hakusalia hata mmoja wao