Niseme Nini ee Bwana

Niseme Nini ee Bwana
Performed by-
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerBernard Mukasa
Views17,944

Niseme Nini ee Bwana Lyrics

  1. Niseme nini ee Bwana, nitamke maneno gani kinywani
    Nikushukuru jinsi gani,
    Nisimulie vipi mimi, mapito niliyopita kuja hapa
    Nikutukuze vipi Mungu
    Niseme tu, Bwana Mungu wangu, asante nakushukuru
    Narudia, Bwana Mungu wangu, asante nakushukuru

  2. Nakumbuka nilivyojaribu, sikujua kama utajibu
    Nikapapasa mkono kizani, kulipokucha ni tunda mkononi
  3. Katikati ya safari maji yale yakamwagika chini
    Lakini kwa wema wako, umeyazoa yakajaa upya
  4. Nilipigwa mawe nikaaibishwa sana
    Tazama leo umeniona, ukamtukuza mtumishi wako