Palikuwa na Kijana Mmoja

Palikuwa na Kijana Mmoja
Performed by-
CategoryWatakatifu
Composer(traditional)
Views6,688

Palikuwa na Kijana Mmoja Lyrics

  1. Palikuwa na kijana mmoja jina lake Samweli,
    Alikuwa akimcha Mungu tangu utoto wake

    Alisikia sauti Ikimwita, Samweli, Samweli *2

  2. Alikuwa 'kiitwa na Mungu, lakini hakujua,
    Alikimbilia kwake Eli, Eli hakuelewa
  3. Aliitwa naye Mungu tena, wala hakufahamu,
    Eli 'kashangaa akasema: Mimi sikukuita
  4. Alipoitwa mara ya tatu, Samweli akajibu:
    Nena, Bwana, mtumishi wako anatega sikio.
  5. Mungu akawa pamoja naye, na Israeli nzima
    Ikafahamu kuwa Samweli ndiye nabii wake