Pendo la Marafiki
| Pendo la Marafiki | |
|---|---|
| Alt Title | Ninyi Ndinyi Mmenikamilisha | 
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Asifiwe Bwana Mungu (Vol 8) | 
| Category | Love | 
| Composer | Martin M. Munywoki | 
| Views | 3,326 | 
Pendo la Marafiki Lyrics
- // u t a n g u l i z i //
 Ninyi ndinyi mmenikamilisha kamilisha (hadi)
 Hadi nikawa hi-vi mi-mi nilivyo (ndugu zangu)
 Ni Mungu Baba ndiye aliyetukutanisha (japo)
 Japo hatulingani tumekamilishana
 {Katika pendo lenu - ndipo nimeelewa jinsi Mungu alivyo
 Nimemuona - Mungu macho kwa macho } *2
 // k i i t i k i o //[ s ] Nikiwa na njaa -
 Ni ninyi marafiki zangu mnimegeao mkate
 [ a ] Penye machungu na maumivu makali -
 Ni ninyi marafiki zangu mwaniuguza majeraha
 [ t ] Nikitawaliwa na hofu -
 Ni ninyi marafiki zangu mnaonipa moyo upya
 [ b ] Tena nikipotea njia -
 Ni ninyi marafiki zangu mwanirudi mwanikosoa
 // m a s h a i r i //
- Ona tunavyosaidiana hima, wenyewe kwa wenyewe,
 Wakati wa furaha hata wa shida
 Tumeweka mbali tofauti kidaraja na mali
 Bahati iliyoje kuwa pamoja
- Ona chuki, wivu, fitina, umimi, havimo kati yetu
 Wakati wa furaha hata wa shida
 Tumeweka msingi imara usiotikisika
 Bahati iliyoje kuwa pamoja
 // h i t i m i s h o //
 { Pendo pendo pendo pendo -
 pendo letu lidumu milele
 Tuombeane tusaidianeni -
 waone Mungu kati yetu } *2
 Wasitenganishwe - wapendanao
 Waombeeni - baraka tele
 sitenganishwe - wapendanao
 Waombeeni - baraka tele, pendo na lidumu
 
  
         
                            