Yesu ni Mwangaza
| Yesu ni Mwangaza | |
|---|---|
|  | |
| Alt Title | Mwangaza | 
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Asifiwe Bwana Mungu (Vol 8) | 
| Category | Injili na Miito (Gospel) | 
| Composer | Bernard Mukasa | 
| Video | Watch on YouTube | 
| Views | 6,078 | 
Yesu ni Mwangaza Lyrics
- Ndipo ukatema mate, aridhini, ukalifanya tope, mkononi
 Ukampaka kipofu , ma-choni, macho yakafunguka, akaona,
 Na mimi ni kipofu, nifumbue, macho ya roho yangu, kwa maana{
 { / s/ Mwangaza ni wewe, Mwokozi ni wewe
 Mwalimu ni wewe, Kiongozi ni wewe
 / w / Ni wewe mwangaza na ni wewe Mwokozi
 Ni wewe mwalimu na ni wewe kiongozi } *2 Yesu
 } *2
- Ukamshusha kutoka, kwenye mti, Yule mtu mfupi, wa ushuru
 Ukala nyumbani mwake, Zakayo, na ukamfundisha, kugeuka
 Naye akakusikia, mwalimu, kageuza mwenendo, kwa maana
- Naomba niongoze, ee Yesu, nibadili mwenendo, nigeuke
 Njia inipotoshayo, niiache, uniponye usugu, wa moyoni
 Dhambi niirudiayo, niishinde, nifundishe niweze, kwa maana
 
  
         
                            